Loading...

Yametimia: SUMAYE Kuwania Uwenyekiti CHADEMA

Akizungumza na wandishi wa habari Kijijini kwake mara baada ya kukabidhiwa fomu ya kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa Kanda ya Pwani na Mwenyeketi wa Dar es Salam, , Kijijini kwake Tondoroni, Kiluvya Pwani, Sumaye, amesema kuwa ni wakati sasa wa kukipeleka chama hicho hadi katika ngazi za vitongiji ambako ndiko wanakoringia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Alisema ni vema watawala wa kiafrika wakawaacha wananchi kutumia demokrasia yao katika kujiamulia kuchagua kiongozi wanayefikiria atatekeleza malengo yao wanayoyatarajia.

“Ndoto niliyo nayo ni ile ile iliyonitoa CCM, katika demokrasia kwa mfano ukienda Marekani huwezi kuona wamarekani wamekiacha CHAMA kimoja kikitawala miaka 30 hadi 40 kwaza hata miaka nane ni bahati sana kwa sababu chama kikitawala miaka nane huwa ni bahati kwasababu wanaju kikishatawala miaka hiyo kitakuwa kimepata fursa ya kutekeleza malengo yake,”amesema Semaye.

Amesema tatizo lilipo Tanzani ni chama kilichopo madarakani kutokubali kuviona vyama vingine vinainua pua ifike pali kwa chama tawala kukubali kushindwa pindi wananchi wanapoamua.

“Kwa kawaida chama chochote kikitawala muda mrefu hakiwezi kufanya vizuri na hiyo ni sawa na anayepiga maji wakati hajui kuogelea hali inayowanyima wananchi fursa ya maendeleo,”alisema Sumaye.

Sumaye, amesema ndoto yake nikuona Chadema ina wafikisha Watanzania kule wanakotaka na kuamini kwamba sasa demokrasia imechukua mkondo wke.

Akizungumzia uchaguzi huo wa Mwenyekiti wa Kanda ya Pwani, Sumaye, amesema anawashukuru wanachama hao kwa kuonesha imani kwake na kuahidi kwamba yuko tayari kufanya kazi ya kukiimarisha chama hicho kuanzia ngazi ya chini kabisa.

Amesema, ingawa ili awe mwenyekiti ni lazima achaguliwe lakini aliwaahidi wanachama hao kwamba Chadema inahitaji kuongoza dola kwa hiyo kazu kubwa iliyoko ni wanachama wa chama hicho kujipanga kuanzia sasa ikiwemo kujiepusha na migogoro isiyokuwa ya lazima.

Amesema haata inapotokea ni vema zikatumika busara katika kuipatia ufumbuzi ambayo matokeo yake ni kuwa na chama imara.

“Nawashukuru kwa kunichangia sh. 100000 ya kunichukulua fomu najuamefanya hivi kwa upendo wenu wala siyo kwa ubaya nami nasema nimekubali ombi lenu Bali naomba mnipigie kura msiishie hapa,”amesema Sumaye.

Naye mwanasheria wake Aidan Kitare amesema kwa vile kesho ndiyo siku ya mwisho atajitahidi pamoja na mgombea wake wanakamilisha utaratibu na kurusisha fomu hiyo kabla ya saa 6:00 mchana.

Mwita waitara mwenyekiti wa Dar es Salaam Kuu aliyekuwepo katika kumsindikiza kiongozi huyo, amesema wanachama hao waliyojitokeza kumchukulia fomu Sumaye walifanya hivyo wakiamini kwamba atakisaidia chama kwa vile anauzoefu mkubwa katika masuala ya uongozi katika utumishi wa Umma.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright CHACHANDU | Designed By AFROPIXELS MEDIA CO. LTD
Back To Top