Loading...

Baby Madaha akanusha kufunga ndoa, alivishwa pete ya uchumba

Msanii wa filamu na muziki, Baby Madaha amekanusha taarifa ambazo zilizagaa katika mitandao ya kijamii kuwa amefunga ndoa na mwarabu wa Dubai.


Mapema mwaka huu gazeti moja kubwa liliripoti taarifa ya kuwa msanii huyo wa filamu alifunga ndoa kimya kimya na mwarabu wa Dubai baada ya ukukubali kubadii dini na kuwa muislam.

Akiongea na Bongo5 Jumanne hii, Baby Madaha alisema kilichofanyika wakati huo ambacho kinadaiwa ilikuwa ni ndoa, ulikuwa ni utambulisho wa mpenzi wake huyo kwa wazazi wake.

“Ndoa bado sijafunga kama baadhi ya watu walivyosema ila nimeveshwa pete ya uchumba na nimemtambulisha mpenzi wangu kwa wazazi” alisema Baby Madaha.

“Kusema kweli kila kitu kinaenda sawa na tayari nimeshavalishwa pete ya uchumba, sema sikutaka kutangaza kwa sababu wasanii wengi wamekuwa wakiishia katika pete za uchumba, kwa hiyo niliona nikishafunga ndoa ndio nitaweka wazi,” aliongeza.

Pia mwigizaji huyo amesema amekubali kubadili dini na kufunga ndoa ya kiislam.

“Unajua sisi wasichana, watu wanasema hatuna dini, kwa hiyo mimi binafsi kama mama yangu akiwa tayari nitafunga ndoa ya kiislam kwa sababu haya ni maisha,” alisema Baby Madaha.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright CHACHANDU | Designed By AFROPIXELS MEDIA CO. LTD
Back To Top